Je? unajua historia ya televisheni hapa Tanzania? na ilipo aanza?


 Zanzibar  televisheni, ndo televisheni ya  kwanza  tena yenye kuonyesha picha za rangi. Televisheni hii ndo ilikuwa ya  kwanza  katika bara  la  Afrika kusini mwa  Sahara. Ilikuwa ikimilikiwa na taifa na niayake ilikuwa nikuleta maendeleo kwa kutumia vipindi vyake. Ilianza mwaka  1972  na ilikuwa inarushwa kwa  Kiswahili na kingereza pia ilibeaba vipindi vya ndani na vya kimataifa. Ilipatikana katika maeneo mbali mbali kama kwenye visiwa vya Unguja na Pemba, pia  signal  zake zilifika hadi  Dar es salaam, Tanga, Bagamoyo pia hadi Mombasa Kenya.
Niaya televisheni ya  Zanzibar  ilikuwa kuelimisha, kuburudisha na kutoa habari. Iliitwa “Televisheni ya kuelimisha” kutokana na wazo  la  Raiswa  Zanzibar  wakati huo ambaye alikuwa Marehemu Abeid  Amin  Karume.
Baadaya  Zanzibar  televisheni huku bara ikanzishwa televisheni nyingine iliyoitwa  ITV(Independence  Television)  ilioanza rasmi mwaka  1994  wakati wa kombe  la dunia. Na  baadaya hii televisheni ikaanzishwa televisheni nyingine ambayo ilikuwa inamilikiwa na taifa iliyoitwa Televisheni ya Taifa (TVT). Hii ilianza kuonekana rasmi mwezi machi  2000  baada ya kumalizika kwa ujenzi wa kituo  pale  kijitonyama jijini  Dar es salaam.  Badae  TVT(TelevisheniyaTaifa) ikabadilishwa na kuitwa  TBC  ambalo jina hilo linatumika hadi sasa.
Vilevile kuna vituo vingine vingi viliazishwa ambavyo ni vya binafsi na vingine vya jamii ambavyo vimeanzishwa katika miji mbali mbali nchini ambavyo hurusha matangazo ya ndani na kutoka nje ya Tanzania  kwa Miktaba Maalum.
Pamoja na kuwa na televeshini zetu wenye bado  tuna  changamoto kubwa kwa mfano bado kuna maeneo mengine kama vijijini haya na huduma ya televisheni. Pia sehemu nyingine zinatumia ungo ilikupata televisheni hizi.Hii ni changa moto kubwa kwa vyombo vya habari haswa  television.
Licha ya televisheni pia kuna vyombo vingine vya habari ambavyo vilianzishwa kama Redio yaTaifa (RTD). Hii Redio  Tanzania  inausikivu  85  katika eneo  la  nchi  la  kilomita za mraba  93970. Pia chombo kingine ni magazeti ambayo mpaka sasa ni magezeti  350  yaliyo sajiriwa lakini  15  tu ya machapisho hayo ambayo yana onekana mitaani kwa wakati huu. Idadi kubwa ya magazeti yaliyo sajiliwa yana milikiwa na watu  au  kampuni binafsi. Ila  “Daily  News”  na “ Sunday News” zinamilikiwa na Serekali chini ya Uongozi wa kampuni ya magazeti ya Serekali (Tanzani Standard Newspaper  Limited).
Vyombo vyote vya habari bado vina changa moto kubwa katika kutumikia watu  wake  na nchi kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment